Uzinduzi wa video mpya "BAADAE" by OMMY DIMPOZI ndani ya NEW MAISHA CLUB
Usiku wa kuamkia leo msanii anayeshikilia tuzo mbili za Kilimanjaro Ommy Dimpozi alikuwa akizindua video yake mpya inayokwenda kwa jina la BAADAE ambayo location zake zilichukuliwa Joz South Africa na video kuzinduliwa Bongo ndani ya New Maisha Club kiwanja cha nyumbani.
Wasanii wenzake walikuwepo kumsindikiza Ommy Dimpozi, msanii kama Chege Chigunda alikuwa mmoja kati ya wasanii waliofanya poa sana na kupata shangwe nyingi hadi kufikia time ya Ommy mwenyewe kupanda katika steji ya Maisha Club
kiatu cha jeshi nini? |
mmmh bila mazoezi huwez kucheza hiyooo |
Dada huyu sikumwelewa kabisa baada ya kupanda katika steji na kuanza kucheza na Ommy si akaanza kuweka mambo hadharani hapo kifuani, katika picha 6 nilizompiga hii ndio inahuwafadhali. Napenda kumwambia kama anajiona hapo siku nyingine awe kidogo na adabu maana na ajitambue yeye ni nani na nyuma yake baada ya kutoka hapo watu watamwelewaje.
No comments:
Post a Comment